Tuesday , 26 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Walimu Hazina kizimbani kwa kuiba mitihani
Habari Mchanganyiko

Walimu Hazina kizimbani kwa kuiba mitihani

Spread the love

PATRICK Cheche, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Kimataifa Hazina pamoja na walimu wanne wa shule hiyo, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa tuhuma za kuvujisha mtihani wa taifa wa darasa la saba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Washtakiwa hao ambao ni pamoja na Mwalimu Mambo Iddi, Laurence Ochieng, Nasri Mohammed na Justus James walisomewa mashataka leo tarehe 26 Septemba 2018 na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Waalimu hao wanadaiwa kuwapa maudhui ya mtihani wa taifa wanafunzi wa darasa la saba wa shule ya Hazina.

Baada ya kusomewa mashtaka, watuhumiwa hao walikana mashtaka wanayodaiwa kufanya tarehe 5 Septemba 2018 kwa kuingilia mtihani wa taifa isivyo halali kwa kuwaonyesha watahiniwa maudhui ya mtihani.

Baada ya watuhumiwa kukana mashtaka, kesi hiyo imepangwa kutajwa tarehe 10 Oktoba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kununua mitambo 15 ya kuchoronga miamba

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Madini imepanga kununua mitambo 15 ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Mtanzania aweka rekodi kimataifa kwa kiwanda cha kusafisha dhahabu

Spread the loveIMEELEZWA kuwa Kiwanda cha Kusafisha dhahabu cha Geita Gold Refinery...

Habari Mchanganyiko

MAIPAC kusaidia Kompyuta shule ya Arusha Alliance

Spread the loveTaasisi ya Wanahabari ya kusaidia Jamii za pembezoni (MAIPAC) imeahidi...

error: Content is protected !!