Serikali mkoani Mtwara imesema ipo tayari kuonesha ushirikiano zaidi na taasisi pamoja na wadau mbalimbali wenye nia thabiti na mipango inayolenga kuwasaidia wanachi katika kuleta maendeleo na kuwakwamua katika umaskini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)
Akizungumza mwishoni mwa wiki mkoani humo wakati wa mnada wa korosho uliombatana hafla fupi ya kukabidhi ya zawadi mbambali kwa wakulima wa korosho mkoa wa Mtwara walioibuka washindi wa droo ya nne ya kampeni ya ‘Vuna Zaidi na NBC Shambani’ Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw Abdallah Malela alitolea mfano ushirikiano uliopo baina ya viongozi wa serikali mkoani humo na benki ya NBC unaosababishwa na namna benki hiyo ilivyo mstari wa mbele katika kuchochea maendeleo sambamba na kuwahudumia vyema wakulima hususani wa zao la korosho.
Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NBC tawi la Masasi Bw Eric Mbeyale alisema kupitia droo hiyo ya nne benki ilitoa zawadi za aina mbalimbali kwa washindi ikiwemo pikipiki, baiskeli, pampu za kupulizia dawa mikorosho, guta, pamoja na zawadi za nyingine ikiwemo kanga, mabegi ya shule na madaftari kwa wakulima mmoja mmoja na AMCOS katika mikoa ya Mtwara na Lindi.
Kwa upande wao washindi wa droo hiyo waliishukuru benki ya NBC kwa kuandaa kwa kampeni hiyo kwa kuwa imekuwa na msaada mkubwa kwao.
Leave a comment