Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakiri kuiba Tausi Ikulu
Habari Mchanganyiko

Wakiri kuiba Tausi Ikulu

Spread the love

WATU watatu wamekiri kuiba ndege watatu aina ya Tausi, wanaodaiwa kuwa mali ya serikali – Ikulu, wenye thamani ya Sh. 3,444,150. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salum Ally wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, watuhumiwa hao Jumatano tarehe 30 Oktoba 2019 wamekubali kulipa fidia.

Imeripotiwa, washtakiwa hao – Mohamed Ally, David Graha na Mohamed Hatibu – wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Julai Mosi 2015 na Oktoba 14, 2019, jijini Dar es Salaam.

Licha ya kulipa fidia hiyo, imeamriwa ndege hao warudishwe serikalini. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amesema, washtakiwa hao wamefikia makubaliano na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) tarehe 28 Oktoba 28 2019.

Mpaka sasa, washtakiwa hao wamelipa fidia 6,890,000 kama hasara waliyosababisha, na kwamba adhabu nyingine kwa mujibu wa sheria zitatolewa na mahakama ndipo waachiwe huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!