Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula
Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love

 

SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza kuwa zaidi ya wakimbizi laki mbili waliopo nchini Tanzania, wataanza kupokea nusu ya mpango wa chakula kuanzia kesho Alhamisi, 1 Juni 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkurugenzi wa WFP nchini Tanzania, Sarah Gordon-Gibson, ameeleza kuwa mgao wa chakula kwa wakimbizi Tanzania, umepunguzwa kwa kasi tangu mwaka 2020.

Taarifa ya Sarah ilinukuliwa na shirika la utangazaji la Ujerumani (DW), jana Jumanne.

Mpango wa Chakula Duniani, WFP limesema kuwa zaidi ya wakimbizi 200,000 nchini Tanzania watapokea nusu tu ya mgao wa chakula kuanzia mwezi ujao kwa sababu ya ukosefu wa pesa za wafadhili.

Wakimbizi watakaoathirika na uhaba huo wa chakula, asilimia 70 wanatoka nchini Burundi na asilimia 30 iliyosalia wanatokea Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).

Kwa muda mrefu sasa, mataifa hayo mawili, yamekuwa yakikabiliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe, huku hali ikiwa mbaya zaidi nchini DRC, kufuatia kuibuka upya kwa makundi ya waasi, yanayoongozwa na wanamgambo wa M23.

Kwa mujibu wa WFP, kuanzia Juni mwaka huu, mgao utapungua kwa asilimia 50, hali inayoweza kuwaacha maelfu ya wakimbizi wakihangaika kukidhi mahitaji yao ya chakula.

Shirika hilo limesema, kunahitajika takribani kiasi cha dola za Marekani 21 milioni (zaidi ya Sh. 50 bilioni), kukabiliana na upungufu wa chakuka.

Sarah amesema shirika hilo lina wasiwasi mkubwa kwamba upunguzaji huo wa chakula, utawalazimisha wakimbizi kuingia katika mazingira magumu zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!