Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wakili wa Nondo awageuzia kibao Polisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Wakili wa Nondo awageuzia kibao Polisi

Spread the love

JESHI la Polisi limetakiwa kufanya upelelezi wa waliohusika kumteka Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wito huo umetolewa na Wakili aliyekuwa anamtetea Nondo katika kesi ya kujiteka, Wakili John Sendodo wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 7 Novemba 2018.

Nondo alishitakiwa kwa kesi ya msingi ya kudanganya kuwa alitekwa na kutoa taarifa za uongo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, kesi ambayo alishinda baada ya mahakama kumkuta hana hatia kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka yake.

“Tunalitaka Jeshi la Polisi kuanza upelelezi wa watekaji waliohusika na utekaji wa Nondo na kuwafikisha katika vyombo vya sheria,” amesema Wakili Sendodo.

Katika hatua nyingine, Mtandao wa Utetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umevitaka vyombo vya dola kuacha kuwakamata watetezi wa haki za binadamu wanapotekeleza majukumu yao na kuwafungulia kesi badala yake kuungana nao katika kuifanya kazi ya utetezi.

“Baadhi ya Viongozi nchini waache kulitumia Jeshi la Polisi kwa kutoa maagizo yanayokwenda kinyume na sheria na utawala bora, Jeshi la Polisi linapaswa kuwa huru na kujitegemea katika kufanya kazi zake,” inaeleza sehemu ya tamko lililotolewa na THRDC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!