Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wakili awalipua wasaidizi wa Rais Magufuli
Habari za Siasa

Wakili awalipua wasaidizi wa Rais Magufuli

John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

WAKILI wa kujitegemea Mchungaji Kuwayawaya Stephen, amesema kuwa viongozi waliopo madarakani katika serikali ya awamu ya tano wengi wao bado hawajaonyesha uwezo wao wa kiutendaji na badala yake wamekuwa wakijificha katika kivuli cha matamko mbalimbali yanayotolewa na Rais John Magufuli, anaandika Mwandishi Wetu.

Kuwayawaya aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake juu ya kusimikwa kwake kuwa Askofu kuongoza huduma inayoitwa Grobal Revival Network.

Amesema kuwa viongozi wengi wa serikali katika awamu ya hii ya tano bado hawajafanya kazi kwa uwezo katika nafasi mbalimbali walizopangiwa na badala yake wengi wao wamekuwa wakifanya kazi kupitia kauli mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na Rais.

Aidha, alisema kuwa viongozi wengi ambao wameteuliwa katika nafasi zao wameshindwa kufanya kazi kwa kujiamini na hivyo kushindwa kuonyesha uwezo wao.

“Kila mmoja anatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sera za eneo lake kwani kila wizara ina sera zake na miongozo yake aliyopewa badala ya kusubiri Ra atoe tamko fulani ndipo wanainukia.

Amesisitiza kwamba changamoto nyingine ambayo anaiona katika utawala wa awamu ya tano ni vitendo vya viongozi kuvujisha siri za serikali hali ambayo haitakiwi kuendelea kufumbiwa macho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!