Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wakili amshauri Rais Samia
Habari za Siasa

Wakili amshauri Rais Samia

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

WAKILI Kuawayawaya Stephen Kuwayawaya, amemshauri Rais Samia Suluhu kuwa makini na watendaji wa ofisi yake. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Kuwayawaya ametoa ushauri huo jana tarehe 29 Aprili 2021, akizungumza na wanahabari jijini Dodoma.

Kuwayawaya amemshauri Rais Samia kuwaondoa watendaji walioko katika ofisi yake, ambao hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.

“Ukimuangalia Samia anaendeshaje nchi unakosea, yeye ni msimamizi na muangalizi, kinachotakiwa kwa Samia ni kuwa na jicho kali kuangalia taasisi yake na waliomo, na kugundua watu wengine ambao hawaendi kwa mujibu wa maelekezo au mwenendo wa taasisi yenyewe, yaani hicho tu akiwa smart  kila kitu kitakwenda vizuri,” amesema Kuwayawaya.

Wakili Stephen Kuwayawaya

Wakili huyo amesema, Rais Samia anapaswa kuwa makini na wasaidizi wake, kwa kuwa ikitokea dosari yoyote atakayenyooshewa kidole ni yeye.

“Rais kama rais ni taasisi, kwa hiyo utendaji kazi wa rais sio utendaji wa mtu mmoja. Yeye anakuwa msimamizi na msemaji wa taasisi, lakini kinachofanya kazi hasa ni watu ambao wako kwenye hiyo taasisi ya rais,” amesema Kuwayawaya.

Samia ambaye ni Rais wa Awamu ya Sita wa Tanzania, aliapishwa kushika nafasi hiyo tarehe 19 Machi 2021, kufuatia kifo cha Hayati Dk. John Magufuli, aliyefariki dunia tarehe 17 Machi 2021, kwenye Hospitali ya Mzena mkoani Dar es Salaam.

1 Comment

  • Yaani kila wakili akitoa ushauri imekuwa ni story?
    Kwanini msitoe maoni ya chama cha mawakili? TLS ni msemaji wa mawakili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!