Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wakazi ataka mchakato Katiba Mpya uendelee
Habari za SiasaTangulizi

Wakazi ataka mchakato Katiba Mpya uendelee

Spread the love

 

MSANII wa HipHop nchini Tanzania, Webiro Wakazi Wassira maarufu ‘Wakazi,’ amesema ni muhimu kuhuisha mchakato wa Katiba Mpya. Anaripoti Matilda Peter…(endelea).

Amesema, anatamani kuona mchakato wa Katiba Mpya unarejea ili maoni ya wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Jaji Joseph Warioba (Mwenyekiti wa Tume), yanafanyiwa kazi.

“Ni muhimu kwa nchi inayohitaji maendeleo kuangalia mchakato wa Katiba Mpya. Nchi inaongozwa na Katiba iliyo huru, Katiba ya Wananchi itasaidia sana kusukuma maendeleo,” amesema Wakazi wakati wa mahojiano na MwanaHALISI TV na Online.

Msanii huyo amesema, Tanzania ina kila sababu ya kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya, hasa kwa kutumia maoni ya wananchi yaliyokusanywa awali.

Amesema, maoni ya wananchi katika Katiba Mpya, yalilenga kutoa mwongozo kwa viongozi na kufinya matumizi mabaya ya madaraka.

“Sasa ni wakati sahihi kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya kwa maslahi ya Taznania na Watanzania,” amesema.

1 Comment

  • Asante ndugu katiba mpya sio muhmu kwetu tunaitaji mafaniko yenye kuleta maendeleo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!