WAUMINI wa kanisa Katoliki leo tarehe 2 Januari, 2023 wameanza kutoa heshima zao mjini Vatican kwa papa mstaafu Benedict XVI, ambaye mwili wake umewekwa katika kanisa la Mtakatifu Petro kwa siku tatu kabla ya mazishi yake.
Kiongozi huyo wa kidini Mjerumani, aliyefariki dunia Jumamosi akiwa na umri wa miaka 95, aliliongoza kanisa katoliki kwa miaka minane kabla ya kuwa papa wa kwanza katika karne sita kujiuzulu mwaka wa 2013.
Mrithi wake Papa Francis ataongoza mazishi Alhamisi wiki hii katika uwanja mkubwa wa Mtume Petro, kabla ya mwili wake kuzikwa katika makaburi yaliyoko chini ya kanisa kuu la Mtume Petro.
Uongozi wa kanisa katoliki mjini Vatican ulitoa jana picha za maiti ya Benedict XVI, akiwa amevalishwa mavazi mekundu ya maombolezo ya upapa na akiwa na kilemba chenye ncha za dhahabu kichwani
Leave a comment