Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wajumbe asilimia 99 CCM watinga Dodoma
Habari za Siasa

Wajumbe asilimia 99 CCM watinga Dodoma

Mkutano Mkuu wa CCM
Spread the love

 

JUMLA ya wanachama wa 1,862 Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho, wamehudhuria mkutano huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Rodrick Mpogolo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara amesema, wajumbe waliotakiwa kuhudhuria mkutano huo leo tarehe 30 Aprili 2021, jijini Dodoma ni 1,876 ambapo idadi kamili ya wajumbe hao huwa 1,909 hivyo kufanya upungufu ya wajumbe 33.

Mpogolo amesema, idadi hiyo ya wajumbe kwa asilimua 99 imefanya akidi iliyohitajika kutimia na kufanya mkutano huo kuwa halali kwa mujibu wa Katiba ya CCM.

Rodrick Mpogolo, Kaimu katibu Mkuu (CCM)

Mpaka sasa, tayari kura za kumchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho imefanyika. Kwenye nafasi hiyo, kuna mgombea mmoja – Samia Suluhu Hassan ambaye ni Rais wa Tanzania. Kura zinahesabiwa.

Uchaguzi mwingine unaoendelea kwenye mkutano huo unaofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete ni wajumbe wawili wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, ili kujana nafasi mbili zlilo wazi.

Tayari kura zimepigwa ambapo wamejitokeza wajumbe sita ambao ni Nguvu Edward Chengula (Iringa), Ashrafu Sadru Kiyokya (Kagera), Kurwa Solo Majiyabululu (Tanga), Happyness Wiliam Mgongo (Dodoma), Fadhili Salum Mgenzi (Kigoma) na Reshma Othman (Kigoma).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!