Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wajane wa Mrisho kuweka kambi kwenye kiwanja
Habari Mchanganyiko

Wajane wa Mrisho kuweka kambi kwenye kiwanja

Wajane na watoto wa Marehemu Mzee Amir Mrisho, wakiwa nje ya Mahakama ya Mwanzo Upanga, Ilala jijini Dar es Salaam
Spread the love

 

WAJANE wa Marehemu Mzee Amir Mrisho, Aseline na Amina Mrisho wamesema ili haki yao ya kumiliki kiwanja namba 108 Port Access isipotee wataweka kambi katika kiwanja hicho kuanzia leo. Anaripoti Selemani Msuya, Dar es Salaam … (endelea).

Uamuzi wa wajane hao kuweka kambi katika kiwanja hicho walichoachiwa na mume wao, umekuja baada ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam, Julieth Dama kutupilia mbali ombi lao ambalo waliomba mahakama hiyo iweke zuio la umilikishwaji wa kiwanja namba 108 kwa mmiliki mpya Kampuni ya Nahla.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya hukumu hiyo wajane hao Aseline na Amina walisema sakata hilo la eneo lao kuuzwa kinyemela limechukua muda mrefu, hivyo wameamua kupambana kwa kila njia ili haki ipatikane.

“Sisi kuanzia sasa tunahamishia vitanda vyetu pale kwenye kiwanja chetu, hatuko tayari kukubali kunyang’anywa kiwanja chetu, ambacho tumeachiwa na mume wetu na watoto wetu 21,” alisema.

Wajane hao walisisitiza kumomboa Rais Samia, Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Anjelina Mabula kuwasaidia kwa kuwa wanaona mahakama zimeshindwa.

“Kinachoonekana kuna mchezo mchafu unafanyika kwenye mahakama zetu, tunaamini Rais Samia na wasaidizi wake wanaweza kutusaidia sisi wajane. Mbaya zaidi hili suala wakati wa uongozi wa Rais John Magufuli lilikuwa kimya baada ya kufa tu limeibuka kwa kasi ya ajabu kuna kitu, sisi hatutakubali, afadhali tufie kwenye kiwanja chetu,” alisema.

Walisema kinachoonekana ni dhahiri kuwa kuna mipango nyuma ya pazia hivyo wanaamini iwapo kutakuwa na uchunguzi wa vyombo vingine ukweli utajulikana.

Wajane hao walisema eneo hilo maarufu kwa Vetenari Mapambano limeajiri vijana zaidi ya miatano ambao wanalipa kodi Serikalini hivyo kuwaondoa kihuni ni jambo ambalo halikubaliki.

Pamoja na wajane hao wanufaika wengine ni watoto wa marehemu Mzee Mrisho ambao ni Omari, Naima, Mariam, Rachel,Rehema, Mrisho, Juma, Zahara, Zainabu, Sharifa, Saidi, Karim, Rajab, Abdul, Hadija, Sauda, Hussein, Ibrahim, Iddi, Riziki  na Sofia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!