Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Waislam wamporomoshea dua JPM
Habari za Siasa

Waislam wamporomoshea dua JPM

Rais John Magufuli
Spread the love

SWALA ya Eid Alhaj iliyoswaliwa kitaifa jijini Dar es Salaam imemalizika kwa kuombewa dua Rais John Magufuli. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Dua hiyo imeendeshwa na Kaimu Mufti, Khatib Jongo mbele ya Waumini wa dini hiyo.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya mgeni rasmi Hussein Alli Mwinyi ambaye ni Waziri wa Ulinzi kufikisha Salam za Eid kutoka kwa Rais Magufuli.

Katika Salam hizo Rais Magufuli aliwaomba masheikh kumwombea dua ili aweze kuongoza kwa amani.

Kauli baada ya maombi hayo, Sheikh Jongo alisimama na kuendesha dua hiyo fupi na kuitikiwa na waumini waliohudhura swala hiyo.

Kwenye Salam zake kwa Waislam, Waziri Mwinyi amesema kuwa, Waislam Ni sehemu muhimu kwa Waislam hivyo jukumu la amani ni muhimu kulitekeleza.

Ameeleza kufurahishwa na uongozi wa Mufti wa Tanzania, Abubakar Zuberi kutokana na kubadili taswira ya baraza hilo.

Amesem kuwa, uamuzi wa Bakwata kujitathmin miongoni mwa mambo muhimu kwenye taasisi hiyo.

Pamoja na mambo mengine Bakwata imepanga kuanzisha viwanda ili kutoa ajira kwa vijana.

Kauli mbiu ya Bakwata chini ya Mufti Zuberi ni Jitambue, Badilika, Acha Mazoea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!