WATUNZI wa Muziki wa Injili nchini wametakiwa kutunga nyimbo zenye ubunifu na maarifa kwa ajili ya utukufu wa Mungu badala ya kutunga nyimbo za hovyo hovyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Mbali na kutakiwa kutunga nyimbo zenye ubunifu pia wametakiwa kujua maana na ulimwengu wa kutumia mziki ambao unaendana na wimbo ulioimbwa kwa kuwa uimbaji unagusa viumbe vyote vilivyopo duniani.
Kauli hiyo ilitolewa na mwalimu wa Muziki wa Injili Dk. Aron Uliyo wakati akitoa mafunzo kwenye semina ya waimbaji wa mziki wa Injili juu ya utunzi na utengenezaji wa muziki wa Injili iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa New Dodoma Hotel Jijini hapa.
Mwalimu Uliyo amesema kuwa muziki ni usanii na sanaa, hivyo ni kipaji ambacho kinatakiwa kutumiwa kwa ustadi mkubwa kwa ajili ya kuweza kutunga wimbo na kutengeneza muziki ambao utaweza kuwa jibu kwa wasikilizani.
“Kazi ya sanaa haitaki kukurupuka inaitaji kuwa na utulivu ili unapokuwa umetunga wimbo lazima uwe na maudhuhi ambayo yanaendana na muziki pamoja na uhusika wa kile kinacholengwa.
“Ikumbukwe kuwa kama utakuwa unaimba wimbo wa kusifu ni lazima uoneshe kusifu, usioneshe ni tofauti na mziki kwani kama itachanganywa itakuwa imepoteza maana,” amefafanua Uliyo.
Katika hatua nyingine amesema kuwa muziki ni zawadi kutoka kwa Mungu na uimbaji na mapigo ya mziki yanaanzia tangu mtoto akiwa tumboni.
Leave a comment