Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wahitimu SUA waomba fedha kununulia vifaa
Habari Mchanganyiko

Wahitimu SUA waomba fedha kununulia vifaa

Daktari wa Mifugo akimtibu ng'ombe
Spread the love

SERIKALI imeombwa kuweka utaratibu wa upatikanaji wa fedha za kununua visanduku vya tiba kwa wanyama na kuweza kumkabidhi kila wanafunzi ili wanafunzi wanaomaliza elimu ya juu ya mifugo waweze kuwa navyo kufuatia kushindwa kufanya kazi vizuri wanapomaliza masomo kutokana na kukosekana kwa visanduku hivyo mahali wanapokwenda. Anaripoti Christina Haule … (endelea).

Ombi hilo lilitolewa jana na mwanzilishi wa kitivo cha tiba ya mifugo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) Prof. Beda Kessy wakati wa sherehe za siku ya tiba ya wanyama duniani iliyofanyika katika viwanja vya hospitali ya wanyama katika ndaki ya tiba ya wanyama na sanyansi za Afya SUA.

Prof. Kessy amesema kuwa mara nyingi wanafunzi hao wamekuwa wakitayarishwa vizuri kielimu wawapo chuoni hapo lakini wanapotoka hapo wakiwa na digrii zao na kuajiriwa kwenye wilaya au maeneo mengine hushindwa kufanya kazi zenye ubora kwa tiba za wanyama kufuatia kukosekana kwa visanduku hivyo.

Hivyo amesema ni vema serikali ingeliona hilo na kutenga bajeti kwa ajili ya manunuzi ya visanduku hivyo kwa manufaa ya wanyama na Taifa kwa ujumla.

Naye Makamu Mkuu wa chuo hicho Prof. Raphael Chibunda amewataka wamiliki wa wanyama kutambua kuwa wao daktari wa mifugo ni muhimu sana kwao na kwa wanyama wao pia.

“Kwa mfugaji iwe ni mbwa, paka, farasi au kuku nafahamu kuwa mnawapenda wanyama wenu lakini kwenu daktari wa mifugo ni muhimu sana kwenu kama alivyo kwa wanyama wake,” amesema.

Amesema kuwa kwa Ndaki ya tiba ya wanyama kujitolea kujitolea kufanya matibabu na ushauri wa bure kwa wamiliki wa wanyama ni nafasi muhimu ya kuzidi kuimarisha mahusiano yao na wanyama na madaktari wao.

Hivyo aliwaomba wamiliki hao kuwa mabalozi wa tiba ya wanyama mahali wanapokaa na kwamba wataalam na vifaa vilivyopo kwa sasa SUA kwa ajili ya Tiba ya mifugo havitumiki kiasi cha kutosha, huku afya za wanyama zikiwa haziko nzuri sana sambamba na magonjwa ya hatari kama kichaa cha mbwa kuendelea kutishia uhai wa binadamu hapa nchini.

Alishauri watanzania wanaoifahamu fursa hiyo kuitua vyema na kuitumia kuwaelimisha watanzania wengi ambao hawajui juu ya uwepo wa taaluma na huduma hizo hapa nchini.

Amesema, ifahamike kwamba uboreshaji wa maisha ya wanyama sit u utawasaidia wanyama na wamiliki wao bali pia itasaidia kuboresha ajira, kuboresha mazao ya wanyama nchini na hivyo kuongeza kipato na uchumi wa nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!