Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wahariri, Waandishi wamsusia Makonda
Habari MchanganyikoTangulizi

Wahariri, Waandishi wamsusia Makonda

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) na Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC), wameazimia kumnyima Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ushirikiano wa kibahari kwa kutoandika au kutangaza habari zote zinazomhusu, anaandika Pendo Omary.

TEF na DCPC wamechukua hatua hiyo, baada ya Makonda kuvamia kituo cha habari cha Clouds Media, kilichopo Mikocheni, kiasi cha saa 5 usiku, Ijumaa ya wiki iliyopita, akifuatana na polisi wenye silaha na kutaka kulazimisha kurushwa kipindi cha SHILAWADU kwa namna atakavyo.

Taarifa ya asasi hizo za wanahabari imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Theophil Makunga, Mwenyekiti wa TEF, na Jane Mihanji, Mwenyekiti wa DCPC, na kuungwa mkono na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

“Kwa pamoja tumeazimia kutoandika habari zote zinazomhusisha Makonda katika vyombo vyetu vya habari. Kwa mantiki hiyo tunamtangaza Paul Makonda kuwa ni adui wa uhuru wa habari na yeyote yule ambaye anashirikiana au atashirikiana naye katika kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa inasema utekelezaji wa azimio hilo unaanza mara moja kwa vyombo vyote vya habari nchini na utaendelea hadi pale itakapotangazwa au kuagizwa vinginevyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!