WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza kuongezeka kwa wagonjwa wapya corona 196, ambapo kati yao kutoka Bara ni 174, Zanzibar 22 na kufanya jumla ya watu waliopata maambukizi kuwa ni 480. Anaripoti Hamis Mguta, Dodoma … (endelea).
Aidha, Majaliwa amesema idadi ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 167, (Zanzibar wako 36, Bara ni 83).
Pia Waziri Mkuu Majaliwa amesema viongezeka vifo vya wagonjwa sita 6, hivyo kufanya jumla ya waliofariki kwa ugonjwa wa Corona kufikia 16 hadi sasa.
Waziri Mkuu ametoa rai kwa Watanzania kuacha kutoa taarifa za uzushi za vifo kuwa kila kifo kinachotokea hakisababishwi na Ugonjwa wa Corona.
Leave a comment