Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Wagonjwa wa corona wafikia 2,474 Kenya, Rais Uhuru asubiriwa
Kimataifa

Wagonjwa wa corona wafikia 2,474 Kenya, Rais Uhuru asubiriwa

Spread the love

SERIKALI ya Kenya imesema, wagonjwa wa corona (COVID-19) nchini huyo wamefikia 2,474. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jana Ijumaa tarehe 5 Juni 2020, Katibu wa Wizara ya Afya wa Kenya, Dk. Mercy Mwangangi alisema idadi hiyo imefikiwa baada ya wagonjwa wapya 134 kukutwa na corona.

Alisema wagonjwa hao wapya 134 ni matokeo ya vipimo vilivyofanywa kwa watu 3,177.

Dk. Mwangangi alisema, kati ya hao 134, watatu ni raia wan je na 131 ni Wakenya. 98 ni wanaume na 36 wanawake.

Alisema hadi jana, watu waliokuwa wamepimwa virusi vya corona walikuwa 90,875.

Dk. Mwangangi alisema, wagonjwa hao 134 wapo katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo ambao ni; Mombasa (67), Nairobi (31), Busia (15), Machakos (5), Taita Taveta (4), Kilifi (2), Nakuru (2), Garissa (1), Murang’a (1), Kisumu (1), Uasin Gishu (1) and Kajiado (1).

Alisema, wagonjwa 51 waliopona corona wameruhusiwa kutoka hospitalini hivyo kufikishwa idadi ya wagonjwa 643 waliopa mpaka jana Ijumaa.

Mtandao wa Worldometer, hadi leo Jumamosi tarehe 6 Juni 2020, umeripoti wagonjwa 3,362,308waliopona duniani, vifo vikiwa 398,535 huku maambukizo yakiwa 6,866,120

Kenya, inasubiri kupata mwelekeo mpya wa jinsi wa kuishi katikati ya janga la corona baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuhutubia Taifa hilo leo Jumamosi.

Wakenya wanasubiri kuona, endapo Rais Uhuru ataregeza masharti ili kuruhusu wananchi kufanya shughuli zao kama kawaida na kupunguza ugumu wa maisha ikiwemo kutoa nafuu ya masuala ya kodi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!