Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wagonjwa wa corona dunia wafikia mil 5.1, vifo laki 3 
Kimataifa

Wagonjwa wa corona dunia wafikia mil 5.1, vifo laki 3 

Takwimu za ugonjwa wa Corona
Spread the love

MAAMBUKIZO ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) yamefikia milioni 5.1 duniani huku vifo vikiwa 330,004. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu ya mtandao wa Worldometer, hadi leo saa 7 mchana ya tarehe 21 Mei, 2020, kati ya wagonjwa hao milioni 5.1, waliopona ugonjwa huo ni milioni 2.03.

Marekani imeendelea kuongeza kwa idadi ya wagonjwa 1.59 milioni sanjari na vifo vikifikia 94,941huku waliopona wakiwa 370,812.

Urusi inashika nafasi ya pili duniani ikiwa na wagonjwa 317,554, vifo 3,099 na waliopona ni 92,681.

Brazili inawagonjwa 293,357, ikiwa nafasi ya tatu kwa wagonjwa wengine huku vigo vikiwa 18,894 na waliopona ni 116,683. Hispania ina wagonjwa 279,524, vifo 27,888 na waliopona ni 196,958.

Uingereza kuna wagonjwa 248,293 na vifo vikifikia 35,704. Nchi ya China ambako ndiko ugonjwa huo ulianzia mwishoni mwa mwaka 2019, ina wagonjwa 82,967, vifo 4,634 na waliopona ni 78,249.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!