Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Maisha Afya Wagonjwa 800 kutibiwa jengo jipya Bugando
Afya

Wagonjwa 800 kutibiwa jengo jipya Bugando

Hospitali ya Bugando
Spread the love

HOSPITALI ya Rufaa ya Bugando (BMC), inatarajia kujenga jengo maalum litakalowahudumia wagonjwa 800 kwa siku ambao wanatibiwa kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), anaandika Moses Mseti.

Hatua hiyo itasaidia kuondoa malalamiko ya muda mrefu yaliyoikuwapo hapo ambayo yalikuwa yanahusiana na msongamano wa wagonjwa.

Kauli hiyo imetolewa leo na Dk. Abel Makubi, Mkurugenzi Mkuu wa BMC, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa jengo hilo linalotarajiwa kuzinduliwa Agousti 25 mwaka huu na Waziri wa afya, Jinsia, Wazee na watoto, Ummy Mwalimu.

Dk. Makubi amesema siku ya uzinduzi huo wananchi watakaofika hospitalini hapo watapimwa baadhi ya magonjwa bure.

Magonjwa yatakayopimwa bure ni pamoja na shinikizo la damu, magonjwa ya sukari, ukimwi, figo, saratani ya kizazi na matiti ili kutoa fursa kwa wakazi wa mikoa ya kanda ya ziwa kufahamu afya zao.

“Lengo ni kuboresha huduma katika hospitali yetu, pia kuhakikisha wagonjwa wanaopata huduma kupitia NHIF wanapata huduma kwa wakati,” amesema Dk. Makubi.

Kelebe Luteli, Mkuu wa Kitengo cha Bima, amesema katika jengo hilo litakuwa na sehemu maalumu kwa viongozi wa kitaifa na kimkoa na kwamba madaktari bingwa wa watoto na wakina mama na wa upasuaji watapatikana muda wowote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Madaktari bingwa 10 waliokuwa India warudi na shuhuda nzito kuhusu utalii tiba

Spread the loveMADAKTARI bingwa wa upasuaji wa ubongo wameendelea kuongezeka katika Taasisi...

Afya

Kipindupindu chabisha hodi Dar, wagonjwa 10 waripotiwa

Spread the love  Ugonjwa wa Kipindupindu umeibuka jijini Dar es salaam ambapo...

Afya

Ujenzi wa zahanati kwa ufadhili wa TASAF wafikia asilimia 95

Spread the love  UJENZI wa mradi wa Zahanati ya Mwanalugali A Kibaha...

Afya

Serikali yatenga Sh. 15 bilioni kukamilisha maboma 300 ya zahanati

Spread the love  SERIKALI imetenga kiasi cha fedha Sh. 15 bilioni, katika...

error: Content is protected !!