SERIKALI ya Kenya imetangaza wagonjwa wapya 124 wa virusi vya corona (Covid-19). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020, Waziri wa Afya nchini humo, Mutahi Kagwe amesema, wagonjwa hao wamebainika baada ya sampuni 2,640 kupimwa ndani ya saa 24 zilizopita.
Kangwe amesema, wagonjwa wamefikia 2,340 nchini humo huku wagonjwa 39 wakipona na wanne wakifariki dunia.
Waziri huyo, amewaomba Wakenya kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo ikiwemo kuepuka mikusanyiko isiyokuwa ya lazima, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji tiririka.
Leave a comment