Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Wagombea Uchaguzi TLS watangazwa, kampeni kuanza Machi 27
Habari Mchanganyiko

Wagombea Uchaguzi TLS watangazwa, kampeni kuanza Machi 27

Wakili Msomi Harold Sungusia
Spread the love

 

KAMATI ya Uchaguzi ya Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), imetangaza majina ya walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika tarehe 12 Mei 2023. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Majina hayo yametangazwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TLS, Charles Rwechungura, baada ya kamati hiyo kuketi kuanzia tarehe 18 hadi 20 Machi mwaka huu, kwa ajili ya kufanya mchujo wa majina ya waliotia nia kugombea nafasi mbalimbali.

Kwa mujibu wa majina hayo yaliyotangazwa hivi karibuni, walioteuliwa kugombea nafasi ya Urais wa TLS, ni Mawakili Wasomi, Harold Sungusia na Reginald Shirima.

Awali waliotia nia walikuwa watatu ambapo jina la Sweetbert Nkuba, lilishindwa kupenya katika mchujo kutokana na kutokidhi vigezo ikiwemo kuwa mtumishi wa umma na kutofanya shughuli za uwakili katika kipindi cha miaka 10.

Wagombea hao wawili waliopenya, watachuana kugombea nafasi hiyo ambayo kwa sasa inashikiliwa na Prof. Edward Hoseah, anayemaliza muda wake.

Kwa upande wa nafasi ya makamu wa rais wa TLS, waliopitishwa kugombea nia, Revocatus Kuuli, Emmanuel Augustino, Aisha Sinda na Fredrick Mtei, huku katika nafasi ya mweka hazina akipitishwa Christopher Mageka, kugombea.

Katika uchaguzi wa mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Vijana, aliyepitishwa kugombea ni Wakili Edward Heche, baada ya aliyekuwa mpinzani wake, Emanuel Nyanza, kuomba kujitoa.

Mawakili Peter Mabiki na Samwel Banzi, wamepitishwa kugombea nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama hicho, huku Susan Reuben akipitishwa kugombea nafasi ya ukatibu.

Taarifa iliyotolewa na Rwechungura, inasema kampeni za uchaguzi huo zitafanyika kuanzia tarehe 27 Machi hadi 11 Mei 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!