Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wagombea CCM ‘matumbo joto’ Dodoma
Habari za Siasa

Wagombea CCM ‘matumbo joto’ Dodoma

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, wakisubiri matokeo baada ya kupiga kura za kumchagua mgombea wa Urais kwa tiketi ya chama hicho
Spread the love

KATIKA kuelekea uchaguzi wa ndani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), baadhi ya wanachama waliochukua fomu kugombea nafasi mbalimbali matumbo yamezidi kupata joto, anaandika Dany Tibason.

Makada hao wanaonekana kujawa na hofu kwa kuwa hawana uhakika kama majina yao yanaweza kurudi hasa kwa wale ambao wanaonekana kuwa na misimamo ya kupinga mwenendo wa chama kwa sasa.

Hofu hiyo imezidi kushika kasi baada ya kauli ya Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali mstaafu, Ngemela Lubinga kueleza kuwa kwa sasa chama kinapitia majina yote ya walioomba nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho.

Lubinga akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumaliziaka kikao cha CCM na viongozi wa Kikoministi cha nchini Vietnam amesema majina ya waombaji kwa nafasi mbalimbali yameanza kupitiwa.

Amesema majina hayo yatapitiwa kabla ya kuyapeleka katika mkutano mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

“Kwa sasa wapo watu ambao wanapitia majina yote ya wagombea ili kufanya mchujo kulingana na sifa kabla hatujayaingia katika mkutano mkuu ambao unatarajiwa kufanyika hivi karibunu, ndiyo maana leo umeona tumekuja hapa wageni ambao ni wajumbe wa kamati kuu kutoka chama cha Kikomonisti nchini Vietnam.

“Na amekuja hapa na timu mbalimbali ya utalii na hiyo ni kutaka kudumisha urafiki wetu na wenzetu na wao wanataka kujifunza mambo mbalimbali ya kilimo pamoja na mambo ya kimazingira bila kusahau kushirikishana mambo ya kisiasa” amesema Lubinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!