Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wagombea 62 ACT-Wazalendo wang’olewa
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wagombea 62 ACT-Wazalendo wang’olewa

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love
JUMLA ya wagombea 62 wa Chama cha ACT-Wazalendo, wameng’olewa kwenye kinyang’anyoro cha ubunge Tanzania Bara na visiwani Zanzibar. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Zitto Kabwe, kiongozi wa chama hicho ametoa kauli hiyo leo tarehe 6 Septemba 2020, jijini Dar es Salaam akieleza kuwa, kadhia hiyo pia imewakumba madiwani wao.

Zitto amedai “wagombea wetu waliondolewa kwa sababu zisizokuwa na mashiko…, nasema hakuna wagombea basi hakuna uchaguzi.

“Tumeteua jumla ya wagombea 168 Tanzania Bara, lakini mpaka sasa wagombea walioruhusiwa kuendelea na kampeni ni 104 tu. Wagombea 24 wa ACT-Wazalendo wameenguliwa na wasimamizi wa uchaguzi na wengine 24 waliwekewa pingamizi.”

Akizungumzia wagombea wa chama hicho Zanzibar amesema, katika majimbo 50 waliyoweka wagombea, jumla ya wagombea 14 wameeunguliwa na katika hao 14, wagombea tisa wanatoka  Pemba.

“Kisiwa cha Pemba kina majimbo 18 pekee, hivyo nusu ya wagombea wetu wameenguliwa na Kisiwa cha Unguja wagombea wetu watano wakienguliwa,” amesema.

Soma zaidi: Zitto ataja kosa la Chadema kwa Lowassa Sumaye

Ametaja baadhi ya sababu zilizochambuliwa na Omar Said Shaaban, mwanasheria wa chama hicho zilizoelezwa na wasimamizi wa uchaguzi ni pamoja na kughushiwa pingamizi kwamba zimetolewa na vyama vingine vya siasa.

Omar Said Shaaban, Mwanasheria wa chama cha ACT-Wazalendo

“Kule Zanzibar kabla hujagombea, lazima muajiriwa aandike barua na uruhusiwe na muajiri wake, sisi tuna ushahidi wagombea wetu wameandika na walipata ruhusa ya muajiri.

Zitto ametaja sababu zingine ni pamoja na wagombea wao kutopokelewa picha za wagombea na baadaye kuwaengua kwa madai ya kutoweka picha kwenye fomu zao.

Amesema, pingamizi zingine zimebuniwa na ofisi za wasimamizi nje ya sheria, wasimamizi kutokuwepo ofisini, kubadilisha maandishi ya wagombea, wasimamizi wa uchaguzi kukataa baadhi ya wadhamini ilhali wapo kwenye daftari la mpiga kura, pia kukaata mihuri ya mahakama, kufanya uamuzi kabla ya majibu ya pingamizi.

Zitto amesema, mchakato wa rufaa unaendelea na kwamba Mwanasheria Mkuu wa chama hicho anafuatalia kwa karibu ikiwa ni pamoja na kuwsasilisha ushahidi wa usio na shaka kwenye maeneo husika.


1 Comment

  • Halafu Profesa Kaabudi eti anamuhakikishia balozi wa Uingereza kuwa uchaguzi eti uko shwari na utaendelea bila matatizo. Nyie mnafikiri hao mabalozi hawaelewi? waangalizi pia wanaelewa na wataandika katika ripoti zao

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!