Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Waganga wa kienyeji mbaroni Mwanza
Habari Mchanganyiko

Waganga wa kienyeji mbaroni Mwanza

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu watatu kwa kosa la kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 8 Agosti 2018, Kamanda wa Polisi Mwanza, DCP Ahmed Msangi watuhumiwa hao, John Luzaria, Masanja Majige na Mariamu Ramadhani, wote wakazi wa Kijiji cha Mahando walikamatwa jana.

DCP Msangi amesema watuhumiwa hao pia walipatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi .

“Watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi na kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali, kitendo ambacho ni kosa kisheria,” amesema DCP Msangi.

DCP Msangi amesema Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na watuhumiwa wote watatu, na kwamba pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamni.

“Aidha upelelezi na msako wa kuwatafuta watu wengine wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali pamoja na upigaji wa ramli chonganishi katika maeneo hayo bado unaendelea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!