Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wafugaji washauriwa kutumia hospitali ya mifugo SUA
Habari Mchanganyiko

Wafugaji washauriwa kutumia hospitali ya mifugo SUA

Spread the love

WAFUGAJI wa mifugo mbalimbali nchini wameshauriwa kutumia hospitali ya Rufaa ya Magonjwa ya Mifugo Tanzania iliyopo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kuwatibu wanyama wanapoumwa ili kuweza kunusuru uhai wao. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Akizungumza kwenye ziara ya baraza la SUA leo tarehe 27 Juni, 2019, Kaimu Rasi wa ndaki ya tiba ya mifugo, Prof. Amandus Muhairwa amesema, hospitali hiyo kwa sasa ina mashine ya Xray mpya, Ultrasound ambayo ni ya rangi pamoja na kuona namna ya kuboresha mashine za ganzi zenye gesi.

Prof. Muhairwa alisema kwa sasa wanasubiri kupata mfadhili wa kusaidia kuendeleza kutoa huduma nzuri zaidi.

Aidha alisema kwa sasa wanautaratibu wa kwenda kuwasaidia wagonjwa wa nje ambao ni wanyama wakubwa wakiwemo ng’ombe kufuatia kutokuwa na eneo kubwa lililoandaliwa kwa ajili yao kwa upasuaji na magonjwa mengine.

Pia alisema, hospitali hiyo hupokea wanyama wanaoumwa hata kutoka katika hifadhi za wanyama nchini na nje yanchi na kutoa huduma za matibabu kwa gharama zinazostahili.

Naye Mkuu wa idara ya upasuaji na uzalishaji wanyama kutoka SUA, Dk. Modesta Makungu aliwashauri wafugaji wanyama wa nyumbani kama mbwa wanaozaa hovyo mitaani kuona haja ya kuwapeleka kufanya upasuaji na kuondoa kizazi.

Dk. Makungu alisema kwa sasa wanafanya oparesheni mbalimbali ikiwemo ya kuondoa kizazi kwa wanyama kabla hawajaanza kuzaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!