Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wafariki dunia wakijipiga ‘Selfie’ kwenye radi
Kimataifa

Wafariki dunia wakijipiga ‘Selfie’ kwenye radi

Spread the love

 

WATU 16 nchini India, wamefariki dunia kwa kupigwa na radi, wakati wakijipiga picha ‘Selfie’. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa mitandao hiyo, tukio hilo limetokea jana Jumapili, katika Mji wa Kitalii wa Jaipur Kaskazini mwa India.

Watu hao wanadaiwa kujipiga picha wakiwa juu ya mnara wa saa maarufu mjini humo, wakati mvua inanyesha.

Inaelezwa kuwa, takribani watu 27 walikuwa juu ya mnara huo wakati tukio hilo linatokea, ambapo baadhi yao walifanikiwa kuruka chini.

Mitandao hiyo imeripoti kuwa, watu wengine 12 wamefariki dunia kwa kupigwa na radi ya umeme, katika majimbo ya Uttar Pradesh na Madhya Pradesh.

Jeshi la Polisi nchini humo limesema kuwa, asilimia kubwa ya waliofariki dunia katika mkasa huo ni vijana.

Inadaiwa kuwa, radi huuwa watu 2,000 kila mwaka nchini India.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!