Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Wafanyabaishara 12 wakamatwa wakiwa na mamilioni ya fedha
Habari Mchanganyiko

Wafanyabaishara 12 wakamatwa wakiwa na mamilioni ya fedha

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Tanga, linawashikilia wafanyabaishara 12 wanaodaiwa kufanya biashara ya ubadilishaji fedha za kigeni bila leseni ya biashara hiyo kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Wafanyabaishara hao walikamatwa katika msako mkali uliofanywa na vyombo vya dola katika maduka ya kubadilisha fedha za kigeni, na maeneo mbalimbali mkoani humo.

Leons Rwegarisa, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Tanga akizungumza na wanahabari tarehe 7 Agosti 2019, amesema jeshi hilo liliwakamata watuhumiwa hao wakiwa na fedha kiasi cha Sh. 63.3 Milioni na Dola za Marekani 65,961.

Kamanda huyo ameeleza, wafanyabiahsra hao wanahojiwa na kwamba uchunguzi wa tuhuma zao ukimalika, watachukuliwa hatua za kisheria.

Wakati huo huo, Kamanda Rwegasira amesema, kwenye operasheni hiyo, jeshi hilo limekamata Paundi ya Uingereza 400, Randi ya Afrika Kusini 1,2020, Euro 270, Shilingi ya Uganda 2,000 na ya Kenya 236,549.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!