Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Waethiopia 25 washikiliwa Kilimanjaro
Habari Mchanganyiko

Waethiopia 25 washikiliwa Kilimanjaro

Spread the love

JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro linawashikilia raia 25 wa Ethiopia waliongia nchini bila ya kufuata sheria. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Waethiopia hao ambao tisa kati yao ni watoto wenye umri chini ya miaka 18, walikamatwa na polisi wakiwa katika kichaka eneo la Himo wakisubiri gari kwa ajili ya kuwavusha kuendelea na safari yao ya Afrika Kusini.

Kamishna Maidizi wa Polisi Hamis Issah, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,amesema raia hao wa Ethiopia walikamatwa na askari Polisi wakati wa doria wakiwa na kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Baraka Itema (25) aliyejitambulisha kama fundi ujenzi .

Kamanda Issah amesema Waethiopia hao wanaendelea kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kwa kusaidiana na jeshi la polisi na kwamba mara baada ya taratibu kukamilika watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili za kuingia nchini bila ya kibali.

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!