Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadau wataka sheria makosa mtandaoni iandikwe upya
Habari Mchanganyiko

Wadau wataka sheria makosa mtandaoni iandikwe upya

Waandishi wa Habari
Spread the love

 

WADAU wa tasnia ya habari nchini Tanzania, wameshauri Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ya mwaka 2015, ifutwe ili kutoa nafasi ya kutungwa upya kwa lengo la kuondoa mapungufu yaliyokuwepo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa kwenye mkutano wa wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali, uliosimamiwa na Jukwaa kwa Wahariri Tanzania (TEF), jana jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhariri wa Gazeti la Majira, Imma Mbuguni, alisema sheria inabidi iandikwe upya Kwa kuwa ilipitishwa kwa dharura bila muswada wake kujadiliwa na wadau kwa ajili ya kutoa mapendekezo ya kuiboresha zaidi.

“Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ifutwe na mchakato wake uanze upya. Sheria hii pamoja na uzito wake, kwanza ilipitishwa kwa hati ya dharura lakini vifungu vyake vingi vinajikita katika dhana,” alisema Mbuguni.

Akizungumza katika mkutano huo, Wakili wa kujitegemea, James Marenga, alisema “Waandishi wanaweza kuweka shinikizo, Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ikafanyiwa marekebisho upya. Vifungu vingi vinajiekeza kwenye dhana, na ni ngumu kuhakiki dhana mahakamani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!