Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadau wa kilimo washauriwa kuzalisha mbegu
Habari Mchanganyiko

Wadau wa kilimo washauriwa kuzalisha mbegu

Spread the love

WADAU wa kilimo na wakulima wakubwa kwa ujumla wameshauriwa kuanzisha makampuni ya mbegu ili kuifanya Sekta ya Mbegu kuwa na uzalishaji wa kutosha kwa mahitaji ya kilimo chenye tija hapa nchini. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Afisa Udhibiti Ubora wa Mbegu kutoka Taasisi ya Kudhibiti ubora wa mbegu Tanzania (TOSCI), Zera Mwankemwa alitoa rai hiyo jana wakati akiongea na mwandishi wa Habari hizi kwenye viwanja vya maonesho ya wakulima vya Mwalimu Nyerere 88 kanda ya Mashariki.

Mwankemwa amesema licha ya kuwepo kwa makampuni zaidi ya 50 yanayozalisha mbegu hapa nchini lakini bado kumekuwa na upungufu mkubwa wa mbegu na kuwafanya wakulima licha ya elimu wanayoipata kujikuta wakitumia mbegu zisizo bora na kupata uzalishaji usio na tija.

“Wakulima hasa wamaeneo ya vijijini baadhi wanajua nini maana ya mbegu bora lakini upatikanaji wake katika maeneo yao unawafanya kushindwa kutumia, na kutumia mfumo wa zamani na kupata uzalishaji kidogo,” amesema.

Amesema, licha ya changamoto za kuanzisha kampuni ya kuzalisha mbegu kuwa ni gharama kubwa lakini, isiwe sababu ya wadau wenye uwezo wa kuanzisha kuacha kujitoa kuanzisha kampuni kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kurudisha nyuma maendeleo ya kilimo nchini.

Mwankemwa amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wakulima wanapata mbegu bora kwa maslahi ya kilimo bora na chenye tija ambapo alisisitiza wadau hao kufika TOSCI kupata maelekezo ya sheria za uanzashaji makampuni ambazo zipo wazi.

Aidha Mwankemwa alisema,TOSCI huwajibika kukagua mashamba ya mbegu ya kila Taasisi au kampuni na kuhakikisha mbegu zinazolimwa zinamwezesha mkulima kupata mbegu bora anayokusudia.

Amesema, sheria ya mbegu ya mwaka 2003 iliyofanyiwa marekebisho yaliyofanyika mwaka 2017 inamuongoza muanzishaji kampuni kusajiliwa na TOSCI huku pia akikaguliwa na TOSCI tofauti na zamani.

Hivyo aliwaomba wakulima kupita kwenye banda la hilo lililopo kwenye maonesho ya wakulima kupata elimu zaidi ya kutambua maana ya mbegu bora na jinsi ya kutofautisha mbegu bora na mbegu feki.

Naye Mkulima mdogo Lucas Simon amesema kuwa kupitia TOSCI ameweza kujifunza namna ya kuandaa mbegu bora sambamba na matumizi ya mbegu bora.

Amesema awali alikuwa na wasiwasi wa matumizi ya mbegu kwani hakuweza kujua mbegu bora ni ipi na feki ni ipi ambapo baada ya kupita kwenye banda hilo amepata uelewa ambao atakwenda kuwafundisha na wakulima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!