Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Wachimbaji madini wapewa somo
Habari Mchanganyiko

Wachimbaji madini wapewa somo

Wachimbaji wadogo wa Dhahabu
Spread the love

WACHIMBAJI wadogo wa madini wametakiwa kuzingatia taratibu za kitalaam wakati wa uchimbaji ili kuepuka ajali  maeneo hayo, anaandika Mwandishi wetu.

Haya yamebainishwa na Mkuu wa mkoa wa Mara Charles Mlingwa wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa tatu wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA),  jijini Mwanza.

Amesema suala la usalama migodini ni muhimu na lazima lizingatiwe katika hatua za mwanzo za uchimbaji.

Amesema ni lazima kuchukua tahadhari katika maeneo ya migodini na kwamba wasiochukua hatua hizo za kulinda usalama serikali itaifungia.

Kwa upande wake Rais wa FEMATA, John Wambura  amesema bado wanakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo za elimu duni ya uchimbaji, uongezaj thamani na uchenjuaji wa madini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!