Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachimbaji Geita waiangukia Serikali ifungue mgodi wao
Habari Mchanganyiko

Wachimbaji Geita waiangukia Serikali ifungue mgodi wao

Spread the love

 

MMILIKI wa shamba lenye machimbo ya madini ya dhahabu, Iddrisa Hussein pamoja na wachimbaji wadogo wa eneo la Mahagi Kijiji cha Izunya Wilayani Nyang’hwale mkoani Geita wameiomba Serikali kufungua mgodi wao kuepusha maduara kujaa maji kutokana na jiografia ya eneo hilo. Anaripoti Paul Kayanda, Geita … (endelea).

Wachimbaji hao wamemuomba Afisa Madini mkazi wa mkoa wa Kimadini Mbogwe, Mhandisi Joseph Kumburu kutazama upya uamuzi wa kusitishwa kwa uzalishaji wa madini hayo.

Amesema badala yake awafungulie ili shughuli za uchimbaji ziendelee na serikali iweze kukusanya mapato yake huku wanakijiji nao wakinufaika na raslimali zilizopo kwenye eneo lao.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa mgodi wa Mahagi, Joseph Yabita amemuomba afisa madini huyo kuharakisha kufungua mgodi huo kwakuwa mwekezaji hana mgogoro na wamiliki wa mashamba pamoja na wachimbaji hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!