Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Wachezaji Simba, Yanga kufturu wakati wa mchezo
Michezo

Wachezaji Simba, Yanga kufturu wakati wa mchezo

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa watani wa jadi (Simba na Yanga) Shirikisho  la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesema kuwa wachezaji wa timu zote mbili watapata nafasi ya kufturu wakati wa mchezo kutokana na baadhi yao kuwa kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhan. Anaripoti Jemima Samwel, DMC … (endelea).

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utapigwa kesho majira ya saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa Habari Afisa Habri wa TFF, Clifford Ndimbo amesema mchezo huo umeangukia kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhan muda utakapofika mchezo utasimamishwa na wachezaji watapata muda wa kufturu kwa waliofunga.

“Wakati huu tupo kwenye mwezi wa Ramdhani na kuna wachezaji wapo kwenye mfungo kwa hiyo katika mchezo wa kesho kutakuwa na mapumziko mafupi ili kuwapa nafasi wachezaji na benchi la ufundi kupata futari,” alisema Afisa Habari huyo.

Aidha katika hatua nyingine Ndimbo, alisema mchezo wa kesho mageti ya uwanja huo yatafungwa majira ya saa 10 jioni, saa moja kabla ya mchezo ili kuepusha usumbufu na kuwataka mashabiki kuwahi mapema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!