Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge waliofariki dunia Tanzania wafikia tisa
Habari za SiasaTangulizi

Wabunge waliofariki dunia Tanzania wafikia tisa

Balozi Dk. Augustine Philip Mahiga
Spread the love

WAZIRI  wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga amefariki dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwake. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Balozi Mahiga ambaye ni mwanadiplomasia mashuhuri anakuwa mbunge wa tisa wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufariki dunia.

Bunge hilo la 11 linaloongozwa na Spika Job Ndugai lilizinduliwa na Rais John Magufuli Novemba 20 mwaka 2015.

Ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Bunge inaonyesha mkutano wa 19 wa Bunge la bajeti ya mwaka 2020/2021 unaoendelea jijini Dodoma utahitimishwa Jumanne ya Juni 30 mwaka 2020 kwa Rais Magufuli kutoa hotuba ya mwisho ya kulifunga.

Wakati uhai wa Bunge ukielekea ukingoni, muhimili huo umejikuta ukipata pigo kwa wabunge wake watatu kufariki dunia katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.

Wabunge hao ni; Dk. Getrude Rwakatare wa Viti Maalum (CCM) aliyefariki dunia Aprili 20, 2020. Dk Rwakatare alikuwa Askofu wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni B, Dar es Salaam.

Mch. Getrude Lwakatare

Majonzi yanayotokana na kifo hicho cha Dk. Rwakatare yakiwa hayajatulia, mbunge mwingine wa Sumve (CCM), Richard Ndassa naye akafariki usiku wa kuamkia tarehe 29 Aprili 2020 akiwa jijini Dodoma.

Taarifa za majonzi kwa muhimili zilianza mwaka mmoja tangu kuzinduliwa kwake kwa Mbunge wa Dimani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hafidh Ali Tahir kufariki dunia tarehe 11 Novemba 2016.

Marehemu Richard Ndassa

Tarehe 31 Machi 2017, DK. Elly Macha aliyekuwa mbunge wa viti maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) alifariki dunia.

Miezi takribani nane baadaye, mbunge wa Songea Mjini kupitia CCM, Leonidas Gama alifariki dunia tarehe 24  Novemba 2017. Tarehe 26 Mei 2018, wananchi wa Buyungu walimpoteza mbunge wao Mwalimu Kasuku Bilago wa Chadema.

Julai 2 mwaka 2018, Mbunge wa Korogwe Vijijini  Steven Ngonyani Maarufu Professa Maji Marefu alifariki.

Tarehe 15 Januri 2020, Mbunge wa Newala Vijijini Rashid Ajali Akbar alifariki dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!