Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wabunge waibana Serikali gharama matibabu figo, Spika atoa maagizo
AfyaHabari za Siasa

Wabunge waibana Serikali gharama matibabu figo, Spika atoa maagizo

Dk. Godwin Mollel, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

 

WABUNGE wa viti maalum, wamehoji mkakati wa Serikali kupunguza gharama za matibabu ya ugonjwa wa figo ili kunusuru wagonjwa wasiokuwa na uwezo wa kumudu hususani gharama za usafishaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akiuliza swali la msingi bungeni leo tarehe 21 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha maswali na majibu, Mbunge Viti Maalum, Mariam Kisangi (CCM), amehoji; Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia wagonjwa wa figo kupata matibabu ya kusafisha figo kwa gharama nafuu?

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel amesema Serikali iko mbioni kukamilisha Muswada wa sheria ya Bima ya Afya kwa wote, ambayo itakuwa suluhisho la kudumu la tatizo hilo.

“Mkakati wa Serikali katika kupunguza gharama za kusafisha figo ni kununua vifaa tiba na vitendanishi moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji, pia Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itakapokamilika itakuwa suluhisho la kudumu,” amesema Dk. Mollel.

Kuhusu wanaotumia bima za afya kutozwa fedha nyingi kupata huduma za kusafisha figo, Dk. Mollel amesema Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, analifanyia kazi suala hilo na kwamba atatoa majibu kuanzia Julai Mosi, 2022.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

“Waziri ameita timu kukaa chini kuangalia namna gani, sio tu kusaidia kwenye vifurushi vikubwa vya bima lakini hata wasio na bima ishuke kabisa hata ikiwezekana iwe Sh. 50,000 kwa mtu mmoja badala ya bei ya Sh. 900,000 kwa wiki ilivyo sasa. Waziri analifanyia kazi muda si mrefu tutapata majibu kuanzia Julai Mosi, 2022,” amesema Dk. Mollel.

Naye Mbunge Viti Maalum, Ghati Chomete, alihoji lini Serikali itapeleka mashine za kusafisha figo katika Hospitali ya Mwalimu Julius Nyerere.

Dk. Mollel amejibu akisema Rais Samia Suluhu Hassan amenunua mashine hizo 171, na kwamba hospitali hiyo itakuwa ni miongoni mwa hospitali zitakazonufaika na mgawo wake.

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mussa Azan Zungu

Kufuatia majadala huo, Naibu Spika wa Bunge, Mussa Zungu, ameishauri Serikali kupunguza gharama za usafishaji figo kwa kuwa mashine zinanunuliwa na Serikali.

“Mnaponunua mashine Sh. bilioni moja, baada ya miaka miwili gharama inarudi kutokana na kuchangiwa. Hamuwezi mkawa mnapunguza gharama za matibabu sababu mashine zinachangiwa na matibabu?” amesema Zungu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!