Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge waibana Serikali ahadi za Magufuli
Habari za Siasa

Wabunge waibana Serikali ahadi za Magufuli

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

SERIKALI imesema itatekeleza ahadi zote zilizotolewa na Rais wa awamu ya tano hayati Dk. John  Magufuli  ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami katika mji wa Bunda. Anaripoti Patricia Kighono,  TUDARCo … (endelea).

Akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Bunda mjini, Robert Maboto (CCM) leo tarehe 3 Septemba, 2021 jijini Dodoma, Naibu Waziri wa nchi, ofisi ya Rais TAMISEMI, David Silinde ahadi hizo zitatekelezwa kama Rais Samia alivyoahidi.

Katika swali la msingi, Maboto aliuliza “Je, ni lini serikali itatekeleza ahadi ya Rais wa awamu ya tano ya ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Bunda kwakuwa mpaka sasa hauna barabara za lami?”

Akijibu swali hilo katika kikao cha nne cha Bunge hilo la 12, Silinde alisema “Serikali inaendelea na mazungumzo na Benki ya Dunia (WB) kutekeleza programu ya uendelezaji miundombinu katika miji unaotarajiwa kutekelezwa katika halmashauri za majiji, manispaa na miji 45 ikiwemo halmashauri ya Bunda mjini.

Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dk. John Magufuli

“Programu hii itahusisha pia ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Bunda kwa kuzingatia vipaumbele vitakavyoainishwa na halmashauri  ya Bunda mjini.

“Serikali itatekeleza ahadi zote za Rais Magufuli kama ilivyoahidiwa na Rais wa awamu ya sita, Samia Suluhu Hassan katika hotuba aliyotoa wakati akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 22 Aprili, 2021.”

Naibu waziri huyo pia ameitaka halmashauri ya Bunda kuweka vipaumbele vya miundombinu wanayotaka serikali ishughulikie ikiwemo ujenzi wa soko kuu la Bunda pamoja na stendi mpya ikiwa ni miongoni mwa ahadi alizozitoa Rais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!