Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wabunge Uingereza wamweka njiapanda waziri mkuu
Kimataifa

Wabunge Uingereza wamweka njiapanda waziri mkuu

Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson anakabiliwa na kitisho katika utawala wake baada ya wabunge kadhaa wa chama chake kupanga kuwasilisha barua za kutaka kuitishwa kwa mchakato wa kura ya kutokuwa na imani naye. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Gazeti maarufu nchini Uingereza, Daily Telegraph limeripoti habari hizo likinukuu duru kutoka ndani ya chama cha Conservatives, ambacho ndicho anachotoka Waziri Mkuu Johnson.

Taarifa zinasema, mpaka sasa, tayari wabunge 20 kutoka chama hicho, wameahidi kuwasilisha barua zao katika wakati hasira ya umma inaongezeka kufuatia ufichuzi kwamba waziri mkuu Johnson alikiuka sheria za kukabiliana na janga la corona.

Kwa mujibu wa taratibu za chama hicho, barua 54 ndiyo zinahitajia kuanzisha mchakato wa kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na duru zinasema idadi hiyo huenda itafikiwa hivi karibuni.

Johnson, Meya wa zamani wa mji wa Londona, analaumiwa kwa kuhudhuria dhifa iliyoandaliwa kwenye ofisi yake ya mtaa wa Downing mwaka 2020, wakati Uingereza ilipokuwa imezuia mikusanyiko yote ya umma ili kuweza kukabiliana na janga la Covid-19.

Johnson alichaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama cha Conservative na aliingia madarakani kumrithi aliyekuwa waziri mkuu wa taifa hilo, Theresa May, Julai mwaka 2019.

Alipata kura 92, 153 dhidi ya aliyekuwa mpinzani wake mkubwa Jeremy Hunt, ambaye alipata kura 46,656, wakati wa mzozo wa kuiondoa Uingereza kwenye Jumuiya ya Ulaya (EU).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!