Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waandishi wa habari watakiwa kutumia sheria kudai haki
Habari Mchanganyiko

Waandishi wa habari watakiwa kutumia sheria kudai haki

Waandishi wa Habari
Spread the love

 

WAANDISHI wa habari nchini Tanzania, wametakiwa kujenga desturi ya kusoma sheria na sera zinazowaongoza ili waweze kuzifahamu kwa lengo la kudai haki zao pindi zitakapokiukwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa leo Alhamisi, tarehe 17 Novemba 2022 na Afisa Uchechemuzi wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Florence Majani, katika mafunzo ya namna ya kuimarisha usawa wa kijinsia katika masuala ya uongozi, iliyoandaliwa na Shirika la Internews na kufanyika mtandaoni.

Florence amesema, mchakato wa maboresho ya sheria zinazosimamia sekta ya habari ukimalika utasaidia kuimarisha haki za waandishi wa habari kwa kuwa sheria bora zitakuwepo, lakini ili haki hizo ziimarike zaidi inabidi wahusika wazifahamu ili waweze kuzisimamia.

“katika mchakato wa maboresho ya sheria za habari watu wanahamasisha sera ziwepo katika vyombo vya habari, zikiwepo zitasaidia mwandishi kujua kwamba mtu akifanya kosa anaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu,” amesema Florence.

Serikali ya Tanzania iko katika hatua za upitiaji maoni yaliyotolewa na wadau mbalimbali kuhusu marekebisho ya sheria za habari, ambapo hivi karibuni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, anatarajiwa kukutana nao kwa ajili ya kupitia maoni yao ili muswada wa mabadiliko hayo upelekwe bungeni kwa hatua za mwisho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!