CHUO Kikuu cha Nairobi kimefungwa kwa muda usiojulikana na Wanafunzi chuoni hapo wameamriwa kuondoka chuoni hapo leo, anaandika Hamis Mguta.
Uamuzi huo umefikiwa na Seneti ya chuo kutokana na suala la kiusalama.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Umma wa chuo hicho, John Orindi amesema, “Tutatangaza ni lini chuo kitafunguliwa.”
Uamuzi huo umechukuliwa kutokana na maandamano yaliyofanyika wiki iliyopita ambayo yalisababisha wanafunzi 27 kujeruhiwa.
Leave a comment