Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Vodacom, Tecno wazindua Camon 20 series, atakayenunua kuzawadiwa GB 96
Habari Mchanganyiko

Vodacom, Tecno wazindua Camon 20 series, atakayenunua kuzawadiwa GB 96

Spread the love


KAMPUNI ya Vodacom Tanzania ikishirikiana na Tecno Tanzania wamezindua simu mpya aina ya Tecno Camon 20 series iliyotengenezwa kwa ubora wa hali ya juu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Simu hiyo yenye uwezo mkubwa katika picha, kutunza chaji, imezinduliwa leo tarehe 20 Mei, 2023 jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Bidhaa za Intaneti wa Vodacom, Samwel Mlelo amesema wana furaha kubwa kujumuika na Tecno Tanzania katika uzinduzi huo wa simu bora kabisa ambayo itasaidia kutimiza lengo lao kama Vodacom la kuhakikisha kila mtanzania anatumia simu bora.

“Vodacom ni zaidi ya kampuni ya simu, hivyo ina lengo la kuhakikisha kila mtanzania anatumia simu bora ambayo itamuwezesha kupata kile anachokitaka, kupitia Tecno Camon 20 series itakata kiu ya mtumiaji wa simu,” alisema Mlelo.

Mlelo alisema Vodacom itamzawadia kila atakayenunua Tecno Camon 20 atapata GB 96 za intaneti bure kwa mwaka mzima ikiwa ni GB 8 kwa kila mwezi.

“Ofa hii itamwezesha mnunuzi wq Tecno Camon 20 kupata GB 96 kwa muda wa mwaka mmoja ambapi ni sawa na GB 8 kwa kika mwezi kutoka Vodacom kwa miezi 12,” alisema Mlelo.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Masoko wa Tecno Tanzania, Salma Shafii amesema wanajuvunia kuzindua simu hiyo ambayo imefanyiwa maboresho makubwa kulingana na matakwa ya wateja wa Tecno.

“Simu hii imekuja na maboresho makubwa katika kamera yake, spidi na uwezo mkubwa wa kuhifadhi chaji,” alisema Salma.

Salma alisema simu ya Tecno Camon 20 series imekuwa na ubora mkubwa ambao umemshawishi msanii mkubwa wa Nigeria, Thiwa Savege ambaye kabla ya kukubali kuwa balozi wa simu hiyo baada ya kukagua ubora wake.

“Kama simu hii ya camon 20 imemshawishi msanii mkubwa barani Afrika, tunakushauri nawe mteja wetu wa Tecno ujaribu simu hii ambqyo tuna uhakika utaridhika na ubora wake,” alisema Salma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!