Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Vjosa Sadriu: Rais mdogo mwanamke duniani aapishwa
Kimataifa

Vjosa Sadriu: Rais mdogo mwanamke duniani aapishwa

Vjosa Osmani-Sadriu rais maya wa Kosovo akikagua gwalide mara baada ya kuapishwa
Spread the love

 

VJOSA Osmani-Sadriu (38), ameapishwa kuwa Rais wa Kosovo, na kaundika historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mwenye umri mdogo duniani kushika wadhifa huo. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Leo tarehe 7 Aprili 2021, Bunge la Kosovo limemuapishwa Sadriu kuwa rais wa taifa hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Awali, Sadriu alichukua madaraka Ikulu muda mchache baada ya aliyekuwa rais wa taifa hilo, Hashim Thaci kujiuzulu kutokana na shinikizo lililobebwa na machafuko na uvunjifu wa haki za binadamu nchini humo.

Hatua ya Bunge la Kosovo lenye wabunge 128, lilimchagua Sadriu kwa kura 71 dhidi ya kura 11 zilizomkataa, kura 38 zilitajwa kuharibika ambapo wabunge wanane hawakupiga kura.

Hata hivyo, wabunge wapinzani walipinga matokeo ya kura hizo wakudai, ulitawaliwa na visa.

Kukimbia ofisi kwa aliyekuwa rais wa taifa hilo – Thaci, kulitoa nafasi kwa Sadriu kutawala Ikulu kuanzia Desemba 2020 mpaka mwishoni mwa Machi 2021, ambapo taratibu za kumpata rais wa miaka mitano ijayo zilipoanza.

Thaci amefikishwa katika Mahakama ya Uhalifu wa Kivita (The Hague), kujibu tuhuma zake kuhusu uhalifu na uvunjifu wa haki za binadamu kwa raia wa Kosovo.

Thaci alianza kuongoza taifa hilo miaka ya 1990 akitoa msituni ambapo aliendesha mpambano ya Kosovo kujiondoa katika utawala wa Serbia.

Uhuru wa Kosovo ulipatikana mwaka 2008 ambapo ulipongezwa na mataifa zaidi ya 100 duniani, hata hivyo Serbia, Urusi na China zilijitenga na pongezi hizo.

Kabla ya kushika wadhifa huo, Sadriu alitoa mchango mkubwa wa mahusiano kati ya taifa hilo na mataifa mengine duniani, lakini aliwahi kuwa mmoja wa viongozi wa juu wa vikosi vya jeshi la nchi hilo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!