Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viti Maalum Chadema pasua kichwa, CC yaahirishwa
Habari za SiasaTangulizi

Viti Maalum Chadema pasua kichwa, CC yaahirishwa

Tundu Lissu, Mgombea Urais Tanzania (Chadema).
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Mendeleo (Chadema) nchini Tanzania, kiko njiapanda juu ya kuamua kupendekeza majina ya wabunge wa viti maalum kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Chadema na Chama tawala-Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndivyo vyenye sifa ya kupendekeza majina ya wabunge wa viti kwa NEC ili iweze kuwateua kuwa wabunge.

Hatua hiyo ni baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumatano ya tarehe 28 Oktoba 2020 na CCM kujikusanyia madiwani na wabunge wengi pamoja na nafasi ya Urais.

Chadema imekuwa katika mjadala mzito ndani na nje ya chama hicho wa je, wapendekeze majina ya wabunge wa viti maalum au isifanye hivyo, hasa ikizingatiwa, imekwisha ueleza umma wa Watanzania kutokubaliana na matokeo ya uchaguzi huo.

Tarehe 31 Oktoba 2020, viongozi wakuu wa Chadema na ACT-Wazalendo, walizungumza na waandishi wa habari na kutaka uitishwe upya uchaguzi mkuu wa Zanzibar na Tanzania kwa kutumia Tume Huru ya Uchaguzi.

Viongozi hao wakiongozwa na wenyeviti, Freeman Mbowe wa Chadema na Maalim Seif Sharif Hamad wa ACT-Wazalendo, walidai uchaguzi huo uligubikwa na ukiukwaji wa sheria, kanuni na miongozo.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema

Kutokana na misimamo hiyo, kumekuwa na mijadala ndani na nje ya Chadema juu ya chama hicho kupeleka majina NEC ya viti maalum ambapo wapo wanaodai yapelekwe na wengine wanasema “kupeleka majina hayo ni kuhalalisha kuwa uchaguzi ulikuwa hauna tatizo.”

Pia, wanadai, kupeleka majina hayo yatakiwezesha chama kupata ruzuku itakayosaidia kuendesha chama huku kikiwa kinajipanga zaidi kwa chaguzi zijazo.

Wapo wanaodai, Chadema ikipeleka wabunge wa viti maalum bungeni, itawawezesha kupata sehemu ya kuzungumzia ndani ya Bunge, ingawa wapo wanaosema “kwenda bungeni, haitakuwa na maana na Chadema itakuwa inajichimbia shimo yenyewe.”

Mbunge mteule wa Nkasi Kaskazini (Chadema), Aida Khenani akijisajili katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Jumapili

Ugumu wa hoja hizo zote, zimeifanya Kamati Kuu ya Chadema (CC), iliyokuwa imekutana jana Jumamosi tarehe 7 Novemba 2020 jijini Dar es Salaam, kujadili masuala mbalimbali ikiwemo hilo ambalo hawakufikia mwafaka na kuamua kuahirisha kikao hadi wakati mwingine.

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, zinadai ni wajumbe wasiozidi saba akiwemo Mbowe, hawataki kupeleka majina NEC kwani wanasema “itakuwa kuwahadaa wananchi, ambao wamewaeleza hawakubaliani na matokeo.”

Mmoja wa wajumbe wa kamati kuu amesema “tumeshindwa kukubaliana bado. Wanaopinga wasiende ni wachache kuliko wanataka waende. Kutokana na hilo, mwenyekiti (Mbowe) aliona ni burasa kuahirisha kikao.”

Amesema, kwa sababu tamko la kutotambua matokeo hayo yalitolewa na vyama viwili- Chadema na ACT-Wazalendo, watajadiliana nao kwanza kabla ya kutoka na uamuzi wa mwisho wa ama kushiriki au la.

Halima Mdee, Mgombea Ubunge wa Kawe kwa tiketi ya Chadema

Katika moja ya andiko la aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu yeye anapingana na kupeleka wabunge wa viti maalum bungeni.

“Nadhani kuna haja ya kutenganisha ‘maslahi ya chama’ na maslahi binafsi ya baadhi ya wanachama wake katika jambo hili. Kila mmoja anadai msimamo wake ni kwa ‘maslahi ya chama.”

Tayari, Katibu wa Bunge la Tanzania, Stephen Kagaigai akizungumza na waandishi wa habari jana Jumamosi alisema kikao cha kwanza cha Bunge Jipya la 12 kitaanza Jumanne tarehe 10 Novemba 2020.

Kagaigai alisema, usajili wa wabunge na taratibu za kibunge, zimeanza jana Jumamosi.

Kwa upande wake, Tundu Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bada) anasema “Ninahisi kuwa kuna baadhi ya watoa hoja, kwa sababu ya nafasi zao, wana fursa ya kufaidika binafsi na uamuzi wa kushiriki bungeni au kwenye halmashauri. Kutokushiriki kutawaathiri wanachama hao moja kwa moja.”

“Hata hivyo, badala ya kukiri kwamba kushiriki kutawapatia faida binafsi na kutokushiriki kutaondoa ‘fursa’ hizo, watu hao wanajificha kwenye kichaka cha ‘maslahi ya chama’!!!”

Lissu anaendelea kusema “Je, chama kina maslahi gani kwenye kuhalalisha uchafuzi wa tarehe 28 Oktoba kwa kukubali kushiriki makombo yanayotokana na karamu ya wachafuzi???. Kama suala ni kukosa ruzuku, tuzungumzie namna ya kutafuta pesa ya ku-replace loss ya hiyo ya ruzuku bila kuhalalisha ubakaji uliofanyika tarehe 28 Oktoba.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!