Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vita dhidi ya Corona: Wanywa bia baa wapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Vita dhidi ya Corona: Wanywa bia baa wapigwa ‘stop’

Spread the love

SOPHIA Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, amepiga marufuku mikusanyiko ya watu katika baa, ikiwa ni sehemu ya hatua za kudhibiti maambukizi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mjema ametoa marufuku hiyo jana tarehe 17 Aprili 2020, na kuelekeza wamiliki wa baa hizo kuhakikisha wateja wao wanaonunua bia, wanakwenda kunywea nyumbani.

Mjema amesema mtu yeyote atakaye kiuka agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

“Waendesha baa mnaelekezwa kuwa vinywaji vitauzwa na mnunuzi atapaswa kunywea nyumbani, na sio kwenye baa. Ni wajibu wa kila mmoja kuzingatia maelekezo haya kwani hatua za kisheria zitachukuliwa kwa mmiliki, muendeshaji na mtu yeyote atakaye onekana kwenye eneo la baa akiendelea kunywa,” amesema Mjema.

Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya COVID-19, ikifuatiwa na Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, jiji hilo lina wagonjwa wapya 38 kati ya wagonjwa 53 walioripotiwa jana katika mikoa saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!