RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kuchukua tahadhari kutokana na kusambaa kwa virusi vya Corona. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).
Akizungumza kwenye uzinduzi wa Karakana Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), leo tarehe 14 Machi 2020 amesema, ugonjwa huo upo, na iwapo kila Mtanzania hatochukua tahadhari yeye na watu wanaomzunguka, ‘tutakwisha.’
“Kila mmoja kwenye familia zetu tutoe tahadhari ya hali ya ugonjwa wa Corona, iwe shuleni, vyuo, makambini na kwenye magari iwe kabla hupanda kwenye dalalala, kondakta atoe elimu kidogo.
“Ndugu zangu waandishi wa habari, ikiwezekana kila siku tutoe ujumbe wa ugonjwa wa Corona, angalau hata kwa maneno matatu. Kwenye TV zetu, kwenye redio zetu, kabla hata hujatangaza taarifa ya habari, pawepo hata mistari miwili ya maneno ya kupambana na Corona, tukidharau ndugu zangu tutakwisha,” amesema Rais Magufuli.
Amesema, tayari nchi nyingi zimetoa tahadhari ikiwa ni pamoja na kuzuia ndege zao kwenda huo, zimeopunguza safari, “ndege yetu iliyoenda India jana, ikirudi leo haitaenda tena.”
“Tuchukue tahadhari, tusipeane mikono, tusibusuane, sifahamu usiku watafanyake, lakini napo unaweza kukwepa usibusu mambo yakawezekana na miraha ikaendelea,’” amesema.
Amesema, anawaomba viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali kuliombea taifa kwa kila mtuna na imani yake huku akisisitiza kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuendelee kusimamia mipaka ya nchi, ili kila anayeingia awe ameangaliwa.
“Tunatambua kuwa Tanzania hatujapata mtu wa ugonjwa huo mpaka sasa, lakini Tanzania hatuwezi tukajiweka pembeni bila kuchukua hatua,” amesema.
Leave a comment