Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Maisha Afya Vipimo vya Dengue kutolewa bure
Afya

Vipimo vya Dengue kutolewa bure

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI imesema vipimo vya homa ya Dengue vitatolewa bure kwa wananchi katika vituo vya afya na hospitali za umma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hayo amesema Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo tarehe 21 Juni 2019 Bungeni Jijini Dodoma wakati akizungumzia hali ya mlipuko wa ugonjwa huo.

Aidha, Ummy amesema serikali itaendelea kuboresha matibabu kwa wagonjwa wa Homa ya Dengue, kwa kuhakikisha dawa za kutosha zinapatikana kwenye vituo vya afya sambamba na kuwajengea uwezo wataalam wa afya.

Hadi sasa, takribani vifo vinne vimeripotiwa kutoka kwa wagonjwa 4,320 waliogundulika kuwa na ugonjwa hu katika mikoa kadhaa, huku Jiji la Dar es Salaam likiwa na wagonjwa 4,029.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Madaktari bingwa 10 waliokuwa India warudi na shuhuda nzito kuhusu utalii tiba

Spread the loveMADAKTARI bingwa wa upasuaji wa ubongo wameendelea kuongezeka katika Taasisi...

Afya

Kipindupindu chabisha hodi Dar, wagonjwa 10 waripotiwa

Spread the love  Ugonjwa wa Kipindupindu umeibuka jijini Dar es salaam ambapo...

Afya

Ujenzi wa zahanati kwa ufadhili wa TASAF wafikia asilimia 95

Spread the love  UJENZI wa mradi wa Zahanati ya Mwanalugali A Kibaha...

Afya

Serikali yatenga Sh. 15 bilioni kukamilisha maboma 300 ya zahanati

Spread the love  SERIKALI imetenga kiasi cha fedha Sh. 15 bilioni, katika...

error: Content is protected !!