Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Vipimo vya corona vyachelewesha mchezo Namungo Vs Nkana
Michezo

Vipimo vya corona vyachelewesha mchezo Namungo Vs Nkana

Spread the love

 

MCHEZO wa Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Namungo FC ya Dar es Salaam, Tanzania na Nkana ya Zambia, umechelewa kuanza kwa dakika 60. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ni baada ya wachezaji wa Nkana, kugomea kupimwa vipimo vya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

Ili kujikinga na maambukizi kwenye michezo ya Kombi la Shirikisho na ile ya Klabu Bingwa Afrika, Shirikisho la Sola Afrika (CAF), limeweka utaratibu wa kupimwa COVID-19, kabla ya mchezo.

Mchezo huo, ulikuwa uanze saa 10:00 jioni katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam leo Jumapili tarehe 4 Aprili 2021, umejikuta ukianza saa 11:00 jioni.

Timu zote mbili, zilitumia takribani dakika nane kupasha misuli kuanzia saa 10:38 hadi saa 10:44 jioni, zikarejea vyumbani kujiandaa kwa mchezo huo wa kundi D.

Haijafahamika haraka makubaliano yaliyofikiwa, hadi kuruhusu mchezo huo kuchezwa pasina timu ya Nkana kupimwa COVID-19.

Timu zingine kwenye kundi hilo ni Pyramid ya Misiri inayoongoza kundi hilo ikiwa na pointi sita sawa na Raja Casablanca ya Morocco lakini zikiwa na tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.

Namungo na Nkana zote hazina pointi yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!