Wednesday , 6 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Viongozi wa dini waombwa kuombea uchaguzi mkuu 2020
Habari Mchanganyiko

Viongozi wa dini waombwa kuombea uchaguzi mkuu 2020

Askofu wa Kanisa la Power of God lililopo eneo la Chanika, Dankon Rwaikila
Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Power of God lililopo eneo la Chanika, Dankon Rwaikila amewaomba watumishi wa dini kumuomba Mungu ili atuchagulie viongozi wenye hofu ya Mungu watakaoweza kujitoa katika nchi yetu ambao wataleta maendeleo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza hayo jana Jumapili tarehe 28 Juni 2020 wakati wa ibada maalumu kwa ajili ya kuwaombea wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari ambapo shule zimefunguliwa leo Jumatatu.

Rwaikila amesema watumishi hao wa dini watakapokuwa na mshikamano wa kumuomba Mungu taifa litapata viongozi wazalendo ambao wenye hofu ya Mungu watakaoweza kujitoa katika nchi yetu.

Pia, maombi hayo yatasaidia kupata viongozi ambao wataweza kuunga juhudi za Rais John Magufuli watakaoweza kutupeleka kwenye ndoto ya Tanzania mpya.

“Ninachojua, jambo zuri linapotaka kutokea shetani anajiinua, hivyo biblia inasema ukimuomba Mungu atatuepusha na mabaya kwenye nchi yetu atupe mshikamano ili tumalize uchaguzi wetu tukiwa na amani na umoja,”amesema Rwaikila.

Waumini wa Kanisa la Power of Godwakiwa kwenye ibada

Pia, amesema wazazi na walezi waendelee kumwamini Mungu kwa kuwa atawalinda watoto wanapokuwa shuleni na Mungu ataendelea kuliokoa taifa na janga hilo la ugonjwa wa Corona.

Wakati huo huo,  Askofu wa Kanisa la Reviral and Praise Fellowship lililopo Chanika, Edmund Kihwili alisema, Mungu ataendelea kuwalinda wanafunzi shuleni kwa kuwa wengi wanahofu wakijua ugonjwa haujaisha hivyo wazazi wanatakiwa wawapeleke watoto wao shuleni.

“Kinachotakiwa kumuamini Mungu na kumthamini, tumeona ushindi na mkono wa bwana umetenda kwa kutuepusha na ugonjwa huu wa Corona,” amesema Kihwili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

error: Content is protected !!