Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Viongozi wa dini Mwanza wataka sheria kali kuwalinda Albino
Habari Mchanganyiko

Viongozi wa dini Mwanza wataka sheria kali kuwalinda Albino

Spread the love

 

KAMATI ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Mwanza, imeiomba Serikali iweke sheria kali na sera za kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), dhidi ya vitendo vya ukatili vinavyofanywa na baadhi ya watu kwa sababu ya imani za kishirikina. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Wito huo umetolewa hivi karibuni na wenyeviti wa kamati hiyo, Askofu Charlea Sekelwa na Sheikh Hassan Kabeke.

“Tunaiomba Serikali iboreshe na kusimamia sheria zinazowalinda watu wenye ualbino. Sheria hizi ziwe madhubutu kiasi kwamba wanapotendewa ukatili wahusika waadhibiwe vikali,” imesema tamko la kamati hiyo.

Wakati huo huo, kamati hiyo imeiomba Serikali kutengeneza sera rafiki zitakazowapa vipaumbele  watu wenye ualbino, ikiwemo kina mama na watoto wenye ualbino katika fursa za kielimu, ajira na mitaji ya ujasiriamali.

“Tunaiomba Serikali ipitishe rasimu ya mwongozo wa utoaji huduma za elimu kwa watu wenye ualbino Tanzania, kupitishwa rasimi hii kutasaidia kuwatengenezea wanafunzi wenye ualbino mazingira jumuishi ya kielimu shuleni,” imesema tamko la kamati hiyo.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo imewaomba wananchi kuripoti matukio ya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watu wenye ualbino, katika vyombo vya dola ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Pia, imezitaka taasisi za dini nchini kutoa mafundisho na elimu kwa jamii, kutoka katika vitabu vitakatifu vya dini, namna Mungu anavyokemea ubaguzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!