Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Vijana 40 wakumbukwa kiuchumi Morogoro
Habari Mchanganyiko

Vijana 40 wakumbukwa kiuchumi Morogoro

Wafanyabiashara mjini Morogoro
Spread the love

MAKUNDI mawili ya vijana wapatao 40 kutoka wilaya ya Kilosa mkoani hapa wamepatiwa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya Sh. 10 milioni ili kujiinua kiuchumi, anaandika Christina Haule.

Akikabidhi msaada huo Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Vijana na Wanawake Mafiga mkoani Morogoro (Mwayodeo), Venance Mlali amesema lengo la shirika hilo ni kuwasaidia vijana wenye umri wa kati ya miaka 18-30.

Amesema vijana hao watasaidiwa kwa kupatiwa elimu ya biashara kupitia mradi wa kuwapa elimu vijana kuhusiana na masuala ya ajira (OYE) na hatimaye kuwaingiza kwenye ujasiliamali na kuwaondoa tatizo la ajira kwa wilaya za Mvomero, Kilosa na Gairo mkoani Morogoro.

Mlali amesema kwamba vikundi vilivyapata vifaa hivyo ni vile vinavyojihusisha na utengenezaji wa majiko sanifu na masuala ya umeme wa jua vyote vikiwa vya wilaya ya Kilosa kutoka kata ya Magole na Ludewa ambavyo vyote vina vijana wapatao 20.

Amesema kuwa kwa ushirikiano na Shirika la Misaada la Uholanzi (SNV), wametoa maboksi ya tochi za aina mbalimbali na vifaa vya umeme wa sola ambao kikundi kimoja kitatumia kuchaji simu za jamii inayowazunguka na kuingiza fedha huku kikundi kingine kikipatiwa seti ya Tv ambayo wataitumia kuonesha picha mbalimbali kwa jamii na kukusanya fedha zitakazowasaidia.

Aidha, amesema makundi hayo yamepewa zawadi hizo kufuatia mashindano ya ujuzi yaliyofanyika mweza Januari mwaka huu huku makundi manne katika wilaya za Kilosa na Mvomero yakishiriki na makundi mawili kutoka katika wilaya ya Kilosa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!