Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari Vigogo ACT mbaroni kwa uchochezi, kukashifu viongozi wa Serikali
HabariSiasa

Vigogo ACT mbaroni kwa uchochezi, kukashifu viongozi wa Serikali

Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini limewakamata na kuwahoji watu wawili ambao ni wanachama wa chama cha ACT Wazalendo kwa tuhuma za kuwakashifu viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kutoa kauli za uchochezi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Viongozi hao walitoa kauli hizo wakiwa katika kikao cha ndani cha chama wakati wakitoa maoni ya kupinga uteuzi wa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Thabit Idrissa Faina.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 11 Disemba, 2022 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa amesema viongozi hao wamekamatwa jana tarehe 10 Disemba, 2022.

Amewataja viongozi hao waliokamatwa kuwa ni Salum Abdalla Herezi maarufu wa Mwalimu Herezi (65) ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya uongozi wa Jimbo la Mtambile mkazi wa Mjimbini.

Mwingine ni Nachia Ali Jamali (39), mjumbe wa kamati ya fedha ya Jimbo la Chambani na mkazi wa Wambaa.

Amesema watuhumiwa hao ambao walitenda makosa hayo tarehe 5 Disemba, 2022 baada ya mahojiano hayo wamechiwa huru na uchunguzi unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariHabari Mchanganyiko

Sekta ya Mawasiliano imekuwa na maendeleo makubwa ya kiuchumi nchini-Mohamed

Spread the loveWaziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Serikali Mapinduzi Zanzibar Khalid...

HabariHabari Mchanganyiko

TCRA yawataka wasafirishaji wa vipeto kujisajili na wengine kuhuisha leseni

Spread the loveMamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Mashariki imetoa wito...

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

error: Content is protected !!