JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini limewakamata na kuwahoji watu wawili ambao ni wanachama wa chama cha ACT Wazalendo kwa tuhuma za kuwakashifu viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kutoa kauli za uchochezi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Viongozi hao walitoa kauli hizo wakiwa katika kikao cha ndani cha chama wakati wakitoa maoni ya kupinga uteuzi wa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Thabit Idrissa Faina.
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 11 Disemba, 2022 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa amesema viongozi hao wamekamatwa jana tarehe 10 Disemba, 2022.
Amewataja viongozi hao waliokamatwa kuwa ni Salum Abdalla Herezi maarufu wa Mwalimu Herezi (65) ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya uongozi wa Jimbo la Mtambile mkazi wa Mjimbini.
Mwingine ni Nachia Ali Jamali (39), mjumbe wa kamati ya fedha ya Jimbo la Chambani na mkazi wa Wambaa.
Amesema watuhumiwa hao ambao walitenda makosa hayo tarehe 5 Disemba, 2022 baada ya mahojiano hayo wamechiwa huru na uchunguzi unaendelea.
Leave a comment